Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Tano 2025 Mkoa wa Geita PDF TAMISEMI Shule walizopangiwa form five 2025 Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) imetangaza orodha ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano kwa mwaka wa masomo 2025. Uchaguzi huu umefanyika kwa kuzingatia matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne uliofanyika mwaka 2024, pamoja na vigezo vilivyowekwa na Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 (toleo la 2023).
Jinsi ya Kuangalia Majina ya Waliochaguliwa
Wazazi, walezi na wanafunzi wanaweza kuangalia majina ya waliochaguliwa kupitia tovuti rasmi ya TAMISEMI kwa kutumia kiungo kifuatacho:
Waliochaguliwa form five Mkoa wa Geita angalia hapa
Sikiliza waziri akitangaza waliochaguliwa kidato cha tano 2025 na vyuo vya kati hapa
Idadi ya Wanafunzi Waliochaguliwa
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na TAMISEMI, Wanafunzi 149,818 sawa na asilimia 69.96 wamechaguliwa kujiunga na masomo ya kidato cha tano, huku 64,323 wakichaguliwa kujiunga na vyuo vya elimu ya ufundi na ualimu.
Jumla ya wanafunzi 214,141 wakiwemo wasichana 97,517 na wavulana 116,624 ilibainishwa wana sifa za kuchaguliwa kujiunga na masomo ya kidato cha tano na vyuo vya elimu ya ufundi ikijumuisha wanafunzi 1,028 wenye mahitaji maalumu.
Kupitia kiungo hicho, unaweza:
- Kutafuta jina la mwanafunzi kwa kutumia namba ya mtihani (Index Number).
- Kuangalia shule aliyopangiwa mwanafunzi.
- Kupata maelekezo ya kujiunga na shule husika.
Maelekezo Muhimu kwa Wanafunzi Waliochaguliwa
Wanafunzi wote waliochaguliwa wanapaswa:
- Kupakua barua za mwaliko fomu za kujiunga na shule (Joining Instructions) kutoka kwenye tovuti ya TAMISEMI au tovuti ya shule husika.
- Kusoma kwa makini maelekezo yaliyomo kwenye barua hizo, ikiwemo tarehe ya kuripoti, mahitaji ya shule na ada (ikiwa inahitajika).
- Kuwasiliana na shule husika kwa maswali au ufafanuzi zaidi.
Hitimisho
TAMISEMI inawapongeza wanafunzi wote waliochaguliwa na inawahimiza kujiandaa vyema kwa ajili ya kuanza safari mpya ya elimu ya sekondari ya juu. Kwa wale ambao hawakupata nafasi katika uchaguzi wa awali, wanashauriwa kufuatilia matangazo ya awamu zinazofuata au kuwasiliana na ofisi za elimu za mikoa na wilaya kwa maelekezo zaidi.
Kwa taarifa zaidi na maswali, unaweza kuwasiliana na TAMISEMI kupitia:
- Barua pepe: ps@tamisemi.go.tz
- Simu: +255 262 321 234
Tovuti rasmi: https://www.tamisemi.go.tz
TAMISEMI inaendelea kujitahidi kuboresha huduma za elimu nchini kwa kuhakikisha kwamba kila mwanafunzi anapata nafasi ya kuendelea na masomo katika ngazi ya juu.
GIPHY App Key not set. Please check settings